Home

BONDIA FRANCIS CHEKA ATIMULIWA NA CHAMA CHAKE

Leave a comment


NDG WAANDISHI WA HABARI   [MICHEZO]

AWALI YA YOTE NINAPENDA KUTOWA SHUKRANI ZANGU ZA DHATI KWENU KWA JINSI AMBAVYO VYOMBO VYENU VYA HABARI VIMEKUWA VIKITUSAIDIA SANA KATIKA KUUKUZA MCHEZO HUU WA NGUMI ZA KULIPWA KWA KUUANDIKA VIZURI SANA NA HATIMAYE KURUDISHA IMANI KUBWA KWA WAPENZI WAKE AMBAO TAYARI WALIKUWA WAMEUKIMBIA KUTOKAN NA SABABU AMBAZO MNAZIFAHAMU FIKA ,NA HATA WADHAMINI KUKAA PEMBENI NA KUUTELEKEZA KABISA.

LKN MIAKA ANGALAU MINNE BAADA YA KUPOTEZA MWELEKEO HATIMAYE MASHABIKI WAMEUPOKEA TENA KWA MIKONO MIWILI ,

HIVI KARIBUNI TAYARI PEPO MBAYA AMEANZA KUJITOKEZA KWA LENGO LA KUUVURUGA TENA MCHEZO HUU AMBAO NI NGUVU KAZI YA VIJANA KTK KUJIPATIA PESA ZA KUJIKIMU KIMAISHA KUPITIA NGUMI ZA KULIPWA.

HIVI KARIBUNI VYOMBO VYENU VYA HABARI VIMEKUWA VIKIRIPOT TAARIFA ZA MVUTANO MKUBWA ULIOJITOKEZA KATI YA BONDIA FRNCIS CHEKA NA WAANDAAJI WA TAMASHA LA USIKU WA MATUMAINI KUHUSU PAMBANO LAKE NA JAPHET KASEBA HUKU CHEKA AKIKANUSHA KWAMBA HAKUSAINI MKATABA WA KUCHEZA NA JAPHET KASEBA NA BADALA YAKE ALISAINISHWA KUPIGANA NA BONDIA KUTOKA MISRI.HAPO TAREHE 07-07-2912 KTK UWANJA WA TAIFA

KIMSINGI TU CHEKA ANAJARIBU KUWAFANYA VIONGOZI WA KAMISHENI YA NGUMI ZA KULIPWA -TPBC HAWAJUWI WAJIBU WAO KWA KUMPA PROMOTA KIBALI CHA KURUHUSU PAMBANO AMBALO NI FEKI WAKATI SIYO KWELI ,

MIMI BANAFSI NILIPATA NAFASI YA KUONGEA NA CHEKA NI KWA NINI ALIPIMA UZITO HALI AKIJUWA HATACHEZA PAMBANO ? NA KWA NINI ALIFIKA UWANJANI HALI AKIJUWA HACHEZI PAMBANO ? ALISHINDWA KUNIJIBU .MAHOJIANO HAQYA TULIYAFANYA SIKU YA PAMBANO NDANI YA UWANJA WA TAIFA.

TPBO INAAMINI KWA DHATI KABISA KWAMBA LENGO LA FRANCIS CHEKA LILIKUWA NI KUJARIBU KUTENGENEZA MAAFA MAKUBWA AMBAYO YANGESABABISHA UVUNJIFU WA AMANI KWA KWA MASHABIKI AMBAO WALIKUJA MAHUSUSI KUANGALIA PAMBANO LILE .

NDG ZANGU WAANDISHI WOTE HEBU JIULIZENI KAMA PAMBANO HILI LINGEKUWA NI LA KAWAIDA NA LIMEPANGWA KUFANYIKA KATIKA UKUMBI WOWOTE ,NA PROMOTA AMESHAWATOZA WATU PESA NA WAMEJAA UKUMBINI ,NA KISHA FRANCIS CHEKA AMEINGIA UKUMBINI NA KISHA KUKATAA KUPIGANA JE MNADHANI MASHABIKI WANGEKUBALI ? NI LAZIMA WANGEFANYA VURUGU KUBWA AMBAYO INGEWEZA HATA KUPTEZA MAISHA YA WATU WENGI SANA NA VYMBO VYENU VYA HABARI VINGEKUWA NA KAZI KUBWA SANA YA KUWAHABARISHA WATANZANIA JUU YA MAAFA HAYO AMBAYO YANGSABABISHWA NA UJINGA WA MTU MMOJA TU FRANCIS CHEKA.

TPBO IMESIKITISHWA SANA NA TUKIO HILI AMBALO LIMEUVUNJIA KABISA HESHIM A MCHEZO HUU ,NA HASA UKUZINGATIA KWAMBA VIKUNDI MBALIMBALI VILISHIRIKI KUCHANGIA UJENZI WA MABWENI A WASICHANA ,NA HATA WAREMBO WALIJITOLEA KUPANDA ULINGONI KWA LENGO LA KUCHANGIA ELIMU.

TPBO INAWAPONGEZA WASANII WOTE WA BONGO MOVIE ,WANAMUZIKI WA AINA ZOTE ,NA WABUNGE WOTE KWA MOYO WAO WA HURUMA WALIOUNYESHA KUFANIKISHA LENGO LA TAMASHA HILO .PIA PONGEZI KWA MABONDIA WOTE WALIOKUBALI KUSHIRIKIKUCHANGIA

BONDIA FRANCIS CHEKA AMESHINDWA KABISA KUWATHAMINI WANAJAMII AMBAO KWA MCHANGO YAO WAMWEZA KUMFANYA AJULIKANE TANZANIA NZIMA ,NA AMEWADHARAU SANA NA AMUVJUNJIA HESHIMA MCHEZO WA NGUMI ZA KULIPWA KWA UJUMLA  WAKE ,NA AMEUDHALILISHA SANA MCHEZO HUU MBELE YA JAMII YA KITANZANIA NA AMEWAFANYA MAADUI WASIOUTAKIA MEMA MCHEZO HUU KWA KUTOKUUDHANINI WAAMINI KWAMBA HUU NI MCHEZO WA WAHUNI NA WAVUTA BANGI .

IMANI ZA TPBO
————-

KUTOKANA NA MAELEZO YOTE NILIYOYATOWA KWENU NI VIZURI PIA MKAJUWA IMANI   ZA TPBO

[1] TPBO INAAMINI KABISA KWAMBA INAAMINIWA NA WATANZANIA WOTE WAPENDAO NGUMI ZA KULIPWA KOTE NCHINI TANZANIA NA INAZINGATIA NIDHAMU NA INAPIGA VITA UTUMIAJI WA MADAWA YA KULEVYA MICHEOZNI ,NA HATA BIASHARA YENYEWE YA MADAWA HAYO. KWA WANAMICHEZO WOTE NCHINI

[2] TPBO INAAMINI KABISA KWAMBA NGUMI ZA KULIPWA NI KAZI KAMA KAZI NYINGINE AMBAZO HUMPATIA BINAADAMU KIPATO CHA HALALI ILI KUJIKIMU KIMAISHA.

[3]TPBO INAAMINI KABISA KWAMBA HAKUNA BONDIA YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU AWEZAYE KIDHARAU JAMII IILYOMZUNGUUKA NA KUFANYA AWEZE KUFANYA MABO AMBAYO YATAIKERA JAMII HIYO .

[4] TPBO INAAMINI KWAMBA KILA BONDIA ANAZO HAKI SAWA ZA KUTETEWA NA KULINDIWA HAKI ZAKE PAKE ZINAPOKUWA HATARINI KUPOTEA.

[5] TPBO INAAMINI KABISA KWAMBA WAKUZAJI [MAPROMOTA] WATAPEWA MSAADA MKUBWA PALE WANAPOANDAA MAPAMBANO YAO NA WANAPATA USHIRIKIANO WA DHATI KUTOKA KWA MABONDIA ,IKWA NI PAMOJA NA KUTANGAZIWA MAPAMBANO YAO KWA USHIRIKIANO MKUBWA NA MABONDIA WAHUSIKA.

[6] TPBO INAAMINI KABISA KWAMBA WAPENZI WA NGUMI ZA KULIPWA WANAZO HAKI ZA KUPATA BURDANI YA MCHEZO HUU IL WAEENDELEE KUUPENDA KWA FAIDA YA MABONDIA WOTE .

[7] TPBO INAAMINI KILA BONDIA ANAPASWA HUHESHIMIWA NA HAKUNA BONDIA ALIYE JUU YA SHERIA NA KANUNI ZA MCHEZO ZIENDESHAZO NGUMI ZA KULIPWA.

NA TPBO INAAMINI KABISA KWAMBA  MWENYE MAMLAKA YA KUBADILISHA MPINZANI WA CHEKA NI PROMOTA NA SIYO BONDIA ,NDIPO CHAMA HUSIKA KINATOWA KIBALI KWA AJILI YA PAMBANO HILO ,NA NDIYO MAANA HATA RAIS WA TPBC KUPITIA VYOMBO VYA HABARI ALIUTANGAZIA UMMA WA WATANZANIA KWAMBA ANAITAMBUWA MKATABA /MIKATABA ALIYOISANI FRANCIS CHEKA KUPAMBANA NA JAPHET KASEBA.

MAAMUZI MAGUMU YA TPBO
—————————

\ KWA KUWA JAMII YA WAPENZI WA NGUMI ZA KULIPWA WAMEFADHAISHWA SANA NA TUKIO LILIOFANYWA NA BONDIA FRANCIS CHEKA NAMI NAUNGANA NAO KTK MFADHAIKO HUO NA KUWAOMBA MSAMAHA KWA TUKIO HILO ,NA ILI KUHAKIKISHA KWAMBA SOTE TUMEFADHAISHWA NA JAMBO HILO-;

TPBO INAMUONDOWA  RASMI BONDIA   FRANCIS CHEKA KATIKA ORODHA YA MABONDIA INAOWATAMBUWA NA HAITAFANYA NAYE KAZI YA IANA YOYOTE KTK ULIMWENGU WA MASUMBWI KTK KIPNDI CHOTE CHA UHAI WA TPBO. NA UHAI WANGU BINAFI.

HII HAINA MAANA KWAMBA ANAKATAZWA KUCHEZA NGUMI ,LA BALI HUU NI MSIMAMO WA TPBO ,NA DAIMA MIMI HUIFANANISHA TPBO NA SIMBA DUME LENYE MENO NA AMBALO HALITAKI KULA MIZOGA , LKN KAMA VIKO VYAMA NINAVYODHANI KWAMBA BILA CHEKA HAVIWEZI KUIMARIKA NA VIMTUMIE SINA PINGAMIZI NAVYO.

TPBO IPO IMARA NA ITAENDELEA KUWA IMARA KWA KUFANYA KAZI NA MABONDIA WENYE NIDHAMU NA KATIKA MAAMUZI YETU HATUMUOGOPI YEYOTE ILI MRADI TUMO NDANI YA SHERIA NA KANUNI ZA MCHEZO

AHSANTENI SANA

NB- KWA TAARIFA HII NINAUFUNGA RASMI MJADALA KUHUSU BONDI FRANCIS CHEKA.

IMEANDIKWA NAMI ;-
YASSIN ABDALLAH -USTAADH

Picha 26 za Pambano dhidi ya Bongo Movies na Bongo Fleva

Leave a comment


This slideshow requires JavaScript.

Mamia kwa maelfu ya wakazi wa jiji la Dar-Es-Salaam na vitongoji vyake walifurika katika uwanja mkuu wa taifa kushuhudia tamasha la burudani mbali mbali za kimuziki, Ndondi pamoja na mpira wa miguu uliohusisha wabunge wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania wanaoshabikia timu za Yanga na Simba, Bongo Flava dhidi ya Bongo Muvi, mpambano wa Wema na Jackline Wolper na mwisho kabisa Ngumi kati ya bondia Japhet Kaseba na Francis Cheka.
Tamasha hilo lililoandaliwa kwa pamoja baina ya Kampuni ya Global Publishers kupitia kitengo chake cha Burudani kwa kutumia platform yao ya ukumbi wa burudani Dar Live, pamoja na mfuko wa elimu na kulipa jina tukio hilo kuwa la Tamasha La Matumaini lilikuwa mahususi kuchangia mfuko wa elimu kwa wasichana katika ujenzi wa mabweni katika shule ya Kongwa mkoani Dodoma…
Watu wa marika mbali mbali walihudhuria tamasha hilo ambalo lilianza rasmi majira ya saa tisa kamili ambapo timu ya Bongo Fleva ilipambana na timu ya Bongo Muvi na timu ya Bongo Fleva kuondoka na ushindi wa goli moja dhidi ya Bongo Fleva katika pambano lililokuwa la kuvutia na vituko pamoja na vibweka kibao. Alikuwa… ambaye aliwainua mashabiki wa Bongo Muvi baada ya kufunga goli katika dakika ya 64 ya kipindi cha pili.
Mastaa kama Claude 112, Steve Nyerere, Abdul Kiba, H baba, TID, Inspector Harun, Vincent Ray kigosi na wengineo walitoa burudani ya kutosha kwa kucheza mpira uliofurahisha na kusisimua wengi. Aidha burudani kubwa ilikuwa baada ya kipyenga cha refa Othman kazi kupulizwa kuashiria mechi imeisha ambapo wachezaji wa Bongo muvi walikwenda kushangilia ushindi kwa mashabiki wao huku wakicheza kwaito na steve Nyerere kuvua jezi yake na kuonyesha maandishi ya “why Always Me? ”. kitendo kilichofanya wamfananishe na Balotelli

sourcebongo5

CHEKA, WOLPER WAAHIDI KUWATWANGA WAPINZANI WAO KWENYE TAMASHA LA MATUMAINI.

Leave a comment


Bondia Francis Cheka (katikati) akitamba mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwa atamchakaza mpinzani wake Japhet Kaseba.

Wolper (kulia) akijitapa kuwa atamtwanga mpinzani wake mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani).

Kocha wa Wema, Rashid Matumla (wa tatu kushoto) akizungumza kwa niaba ya Wema (ambaye hakuwepo) kwenye mkutano huo.

Nahodha wa Bongo Fleva, H Baba (kulia) akiahidi ushindi kwa timu yake dhidi ya Bongo Movie.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na (kutoka kushoto) kocha wa bondia Francis Cheka (Abdalah Saleh Komando), Francis Cheka, meneja wa mfuko wa elimu (Charles Kapima), mmoja wa waratibu wa tamasha hilo (Luqman Maloto), promota wa pambano hilo, Kaike Silaju, bondia Japhet Kaseba na mwisho ni meneja wa Kaseba (Idd Bakari).

Wakati homa ya mapambano ya ndondi yanayosubiriwa kwa hamu kati ya Francis Cheka na Japhet Kaseba pamoja na wakali wa filamu nchini, Wema Sepetu na Jacqueline Wolper, ikizidi kupanda, baadhi ya mabondia hao wametoa tambo kuwa watawachakaza wapinzani wao siku hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya kisasa ya The Atriums jijini Dar, Jacqueline Wolper alitamba kumpiga vibaya mpinzani wake siku ya Jumamosi kwenye Tamasha la Matumaini pale Uwanja wa Taifa.
“Sipendi maneno, napenda vitendo, nimekuwa nikisikia Wema na rafiki yake wanaongea sana kuhusu mimi kwenye TV.
“Nataka nikate mdomo wake siku hiyo kwa kumpiga” alisema Wolper. Nae Bondia Francis Cheka alitamba kuwa kama kawaida yake atamchachafya mpinzani wake katika tamasha hilo.

source:PICHA/HABARI : ERICK EVARIST/GPL

Japheratz kaseba kuzipiga na Francis

Leave a comment


Mabondia, Francis Cheka (kushoto) na Japhert Kaseba, wakitunishiana misuli wakati wa utambulisho wa mpambano wao unaotarajia kufanyika Siku ya tarehe saba mwezi wa saba katika uwanja mpya wa taifa ambapo kutakuwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii nchini wakiongozwa na Diamond pia kutakua na mechi ya Bongo Move na wasanii wa Bongo Fleva watakapochuana kwa mara nyingine katika mpambano uho ulioandaliwa na Global na kuratibiwa na Kaike Siraju utakuwa ni mpambano wa kwanza wa Masumbwi kufanyika katika uwanja mpya wa Taifa


Baadhi ya mabondia watakaosindikiza mpamnbano huo ni Adiphoce Mchumia tumo atakaedundana na Ramadhani Kido wakati Amos Mwamakula ataoneshana kazi na Rashini Ali uku Mkongo Kanda Kabongo akizipiga na Said Mbelwa wakati bondia chipkizi kutoka kambi ya masumbwi ya Ilala inayonolewa na Kocha Mkongwe Habibu Kinyogoli Masta na Kocha maarufu Rajabu Mhamila ‘Super D’ watampandisha bondia Ibrahimu Class kuoneshana kazi na Sadiki Momba

Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis na wengine kiba DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

source;josephatlukaza.blogspot.com